Manchester United wameamka, Maguire 🔥


 KWANZA ALAMA 3 ...! 


✍🏻Manchester United walifanya vitu vingi sana kwa usahihi na mpango wa kocha ulifanikiwa shida ilikuwa kufunga magoli mengi na ndio maana hata goal difference ya United inaelezea 


✍🏻Mpango ulikuwa :- 


1: Tanua ile back 5 ya Luton kwa Garnacho na Rashy kuwa pembeni zaidi ya uwanja ili .... 


2: Kutengeneza space katikati ya wingbacks na outside CBs wa Luton kuishambulia 


3: Kuwa na idadi kubwa ya wachezaji pembeni ya uwanja dhidi ya wingbacks wao ( Garnacho + Reguilon Vs Kabore na Rashy + Dalot Vs Alfie ) ili kuwa na mchezaji mmoja zaidi ( create overloads ) 


4: Kulazimisha Luton kupoteza mpira haraka mara tu baada ya kuupata ( forced turnovers ) 


5:Kilichowakwamisha United kutofunga magoli mengi ni umaliziaji wao tu leo ... ulikuwa mbovu 


✍🏻Luton mpango wao ulikuwa mmoja tu , kuhakikisha wanazuia kwa idadi kubwa ya wachezaji , kufunga njia za katikati ya uwanja na kusubiria 


1: Counter attacks 

2: Mipira iliyokufa tu . 


NOTE 


1: Maguire tangu amerejea kikosini anacheza vizuri 


2: Umaliziajia kwa United ni shida kubwa sana msimu huu mpaka sasa 


3: Chong sijui kwanini alianzia bench , maana alivyoingia aliwapa tabu sana United hasa nyuma ya kiungo chao 


4: Hojlund akae chini amalize tofauti zake na EPL , nafasi zile zile anapata UCL anaweka kambani lakini EPL anakosa . Mechi 9 hana goli wala assist . 


5: Wanatamani kusema Luton wepesi lakini wakikumbuka walipata sare inabidi wasonye tu 😀😀😀


FT: Man United 1-0 Luton

No comments