JACOB ZUMA AIOMBA MAHAKAMA IBATILISHE KIFUNGO CHAKE

Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma  ameiomba Mahakama kuu nchini humo kubatilisha kifungo chake cha miezi 15 jela kwa kukosa kufika kwenye uchunguzi wa ufisadi, akisema wameshtukiza na isiyo ya haki na inaweza kumuua kutokana na janga la COVID-19 akiwa gerezani.

Mahakama ya katiba ilimhukumu Zuma kifungo cha miezi 15 jela Jumanne kwa kukosa kufika katika uchunguzi wa ufisadi ulioongozwa na Naibu Jaji Mkuu Raymond Zondo mnamo Februari. 

Alipewa siku tano kufika mbele ya polisi, lakini haikujulikana ikiwa ataenda kwa hiari. 

Wafuasi wake wamekusanyika katika mji wa Nkandla nchini humo kupinga kukamatwa kwake.

No comments