AMKA NA BWANA LEO 6

*KESHA LA ASUBUHI.*

Jumanne, 06/07/2021.

*LIHUBIRI NENO.*

*Msiseme, Ni fitina, katika habari za mambo yote ambayo watu hawa watasema, Ni fitina; msihofu kwa hofu yao, wala msiogope. Isaya 8:12.*

▶️Kazi yetu ni kutangaza kwa ulimwengu ujumbe wa malaika wa kwanza, wa pili, na wa tatu. Katika kutekeleza wajibu wetu, hatupaswi kuwadharau au kuwaogopa adui zetu. Kujifunga kwa mikataba na wale wasio na imani yetu sio mpango wa Mungu.

▶️Tunapaswa kuwatendea kwa wema na heshima  wale wanaokataa kuwa waaminifu kwa Mungu, lakini hatupaswi  kwamwe, kuungana nao katika shauri, juu ya masilahi muhimu ya kazi ya Yake, kwani hii siyo njia ya Bwana. Tukiweka tumaini letu kwa Mungu, tunapaswa kusonga mbele kwa uthabiti, tukifanya kazi yake bila ubinafsi, kwa kumtegemea Yeye kwa unyenyekevu, tukijikabidhi sisi wenyewe na yote yanayotuhusu wakati wetu wa sasa na wa badaye kwa majaliwa ya Yake ya hekima, tukishikilia mwanzo wa wa imani yetu kwa uthabiti hadi mwisho, tukikumbuka kuwa sio kwa sababu ya kustahili kwetu ndio tunapokea baraka za mbingu, bali ni kwa sababu ya kustahili kwa Kristo, na ukubali wetu, kwa njia ya imani kwake Yeye, wa neema ya Mungu iliyo tele.

▶️Ninaomba kwamba ndugu zangu watambue kuwa ujumbe wa malaika wa tatu una maana sana kwetu, na kwamba utunzaji wa Sabato ya kweli unapaswa kuwa ishara inayotofautisha wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia Yeye. Hebu na waamke wanaosinzia na wasiojali. Tunaitwa kuwa watakatifu, na kwa uangalifu tunapaswa kuepuka kutoa picha kwamba haina faida yoyote ikiwa tutadumisha sifa za pekee za imani yetu au hapana. Juu yetu tunao wajibu mzito wa kuwa na msimamo thabiti zaidi kwa ajili ya ukweli na haki kuliko vile tulivyokuwa huko nyuma.

▶️ *Mstari wa mpaka kati ya wale wanaoshika amri za Mungu na wale wasiozishika, unapaswa kudhihirishwa kwa uwazi kabisa. Tunapaswa kumheshimu Mungu kwa makini, tukitumia kwa bidii kila njia ya kudumu kuwa katika uhusiano wa agano pamoja naye, ili tuweze kupata baraka Zake—baraka ambazo ni za muhimu sana kwa watu ambao watapitia katika majaribu makali sana. Kuashiria kuwa imani yetu, dini yetu, sio nguvu inayotawala maishani mwetu, ni kumvunjia Mungu heshima sana.*

*MUNGU ATUBARIKI SOTE*

No comments