ABDUL NONDO; WALIKATAA KUNIPA USHIRIKIANO
Barua yangu ilijibiwa tar 15 ,Novemba 2019 ,wakikataa kunipa ushirikiano kukagua Daftari la Makonda nilijua tuu ni kwasababu ya hofu iliyokuwepo na namna Makonda alivyokuwa anaogopwa . Ila suala la kukagua Daftari la mtumishi wa umma katika ofisi ya Sekretariati ya maadili haipaswi kuwa suala la kuomba au la siri, kiongozi akishakuwa mtumishi wa umma tuu kila kitu kuhusu utumishi wake kinapaswa kiwe wazi na umma ujue.
Nitumie fursa hii mara nyingine kwa mujibu wa Sheria ya Takukuru Na.11 ya 2007 kifungu cha 39 kinachonipa mimi mamlaka kama mwananchi kutoa taarifa kwa TAKUKURU popote ninapoona kuna maksio ya uwepo wa Rushwa , kutokana na tuhuma kuwa nyingi dhidi ya Paul Makonda ni vyema TAKUKURU imchunguze na Makonda ili kujiridhisha .
Na kazi ya kuchunguza na kujiridhisha (Prove or disprove the allegations) ni kazi yenu TAKUKURU kama ilivyoelezwa katika sheria ya TAKUKURU kifungu cha 7(e),(f),i,ii,iii, na cha 10 (1) a,b,c .
Sasa tunashangaa kuona mnakanusha kutomkamata Paul Makonda wala kumchunguza.
Nitumie fursa hii mara nyingine kwa mujibu wa Sheria ya Takukuru Na.11 ya 2007 kifungu cha 39 kinachonipa mimi mamlaka kama mwananchi kutoa taarifa kwa TAKUKURU popote ninapoona kuna maksio ya uwepo wa Rushwa , kutokana na tuhuma kuwa nyingi dhidi ya Paul Makonda ni vyema TAKUKURU imchunguze na Makonda ili kujiridhisha .
Na kazi ya kuchunguza na kujiridhisha (Prove or disprove the allegations) ni kazi yenu TAKUKURU kama ilivyoelezwa katika sheria ya TAKUKURU kifungu cha 7(e),(f),i,ii,iii, na cha 10 (1) a,b,c .
Sasa tunashangaa kuona mnakanusha kutomkamata Paul Makonda wala kumchunguza.
Post a Comment