ABDUL NONDO; MAKONDA ALITOA WAPI HELA?
Tuhuma zingine zilitolewa katika Blog ya Mtandao ya Sauti Kubwa inayomilikiwa na Ansbert Ngurumo ,mnamo tar 30 Agosti 2018 aliandika na kuambatanisha na nyaraka mbalimbali za umiliki wa viwanja kwamba Makonda ana miliki Ardhi Dodoma eneo la Iyumbu new Town Center viwanja sita jumla mita za mraba 92,341 .
Pia Kugawa gawa fedha.
Tarehe 3/Juni/2019 alitoa fedha kwa wachezaji wa Simba milion 10 kwa Golikipa Manula,milion moja moja kwa kila mchezaji,milion mbili kwa mchezaji wa kike,milion 3 kwa msemaji wa simba @hajismanara na septemba 9,2019 akatoa milion 10 kwa Juma Kaseja ,tar 5 Oktoba 2019 uwanja wa uhuru Dar alitoa Shiling Mil.100 kwa wajumbe wa shina wa CCM Mkoa wa Dar.(Chanzo Millard Ayo na EATV).
@takukuru.tz
mmewahi waza fedha hizi alitoa wapi ? kwamba ulikuwa mshahara wake wa mfukoni ?
Tarehe 18/Septemba/2019 siku ya Jumaano kupitia Gazeti la Mwananchi iliandika kichwa cha habari "Makonda aeleza anakotoa fedha". Makonda kwa kauli yake ya mdomoni baada ya watu kuhoji wapi anapata fedha hizo zote za kugawa gawa ikiwa yeye ni mkuu wa mkoa tuu.
Katika taarifa hii alisema yeye anatumia watu wenye kipato kikubwa kuwaelezea shida na wao hutoa msaada akitolea mfano milion 10 alizompa Juma Kaseja , Makonda alijibu pia nchi hii ni tajiri na watu wake ni matajiri .Kama fedha alikuwa anapewa na wahisani au marafiki je sheria ya inasemaje mtumishi wa umma anapopokea zawadi ? .
Sheria ya maadili ya viongozi wa umma Na. 13 ya 1995 kama ilivyofanyiwa marekebisho kuanzia kifungu cha 12(2 na 3) inaeleza utaratibu wa mtumishi wa umma kupokea zawadi ya zaidi ya thamani ya laki mbili, alipaswa kutoa taarifa kwa muajiri wake lakini pia taarifa ya matamko ya zawadi alizopewa yanapaswa kuwepo katika ofisi ya Kamishna Sekretariati ya Maadili.
Na ndio maana tar 17, Oktoba ,2019 niliandika Barua Sekretariati ya Maadili chini ya Kamishna wa maadili ya viongozi wa umma Marehemu Jaji Mstaafu Harold R. Nsekela nikiomba kukagua Daftari la Maslahi , Rasilimali na madeni pamoja na matamko ya zawadi ya Makonda kama ambavyo kanuni za maadili ya viongozi wa umma za 1996 Na. 168 kifungu cha 6 na 7 kinavyoniruhusu mimi kama Raia kuomba kukagua Daftari hilo.
Pia Kugawa gawa fedha.
Tarehe 3/Juni/2019 alitoa fedha kwa wachezaji wa Simba milion 10 kwa Golikipa Manula,milion moja moja kwa kila mchezaji,milion mbili kwa mchezaji wa kike,milion 3 kwa msemaji wa simba @hajismanara na septemba 9,2019 akatoa milion 10 kwa Juma Kaseja ,tar 5 Oktoba 2019 uwanja wa uhuru Dar alitoa Shiling Mil.100 kwa wajumbe wa shina wa CCM Mkoa wa Dar.(Chanzo Millard Ayo na EATV).
@takukuru.tz
mmewahi waza fedha hizi alitoa wapi ? kwamba ulikuwa mshahara wake wa mfukoni ?
Tarehe 18/Septemba/2019 siku ya Jumaano kupitia Gazeti la Mwananchi iliandika kichwa cha habari "Makonda aeleza anakotoa fedha". Makonda kwa kauli yake ya mdomoni baada ya watu kuhoji wapi anapata fedha hizo zote za kugawa gawa ikiwa yeye ni mkuu wa mkoa tuu.
Katika taarifa hii alisema yeye anatumia watu wenye kipato kikubwa kuwaelezea shida na wao hutoa msaada akitolea mfano milion 10 alizompa Juma Kaseja , Makonda alijibu pia nchi hii ni tajiri na watu wake ni matajiri .Kama fedha alikuwa anapewa na wahisani au marafiki je sheria ya inasemaje mtumishi wa umma anapopokea zawadi ? .
Sheria ya maadili ya viongozi wa umma Na. 13 ya 1995 kama ilivyofanyiwa marekebisho kuanzia kifungu cha 12(2 na 3) inaeleza utaratibu wa mtumishi wa umma kupokea zawadi ya zaidi ya thamani ya laki mbili, alipaswa kutoa taarifa kwa muajiri wake lakini pia taarifa ya matamko ya zawadi alizopewa yanapaswa kuwepo katika ofisi ya Kamishna Sekretariati ya Maadili.
Na ndio maana tar 17, Oktoba ,2019 niliandika Barua Sekretariati ya Maadili chini ya Kamishna wa maadili ya viongozi wa umma Marehemu Jaji Mstaafu Harold R. Nsekela nikiomba kukagua Daftari la Maslahi , Rasilimali na madeni pamoja na matamko ya zawadi ya Makonda kama ambavyo kanuni za maadili ya viongozi wa umma za 1996 Na. 168 kifungu cha 6 na 7 kinavyoniruhusu mimi kama Raia kuomba kukagua Daftari hilo.
Post a Comment