• HOME
  • BREAKING NEWS
  • TAMTHILIA
  • MICHEZO
  • MATANGAZO
  • CONTACT US

BINAGO BLOG

  • Home
  • Home / Habari / HUSSEIN MWINYI; ZANZIBAR MUACHE TABIA YA MUHALI

    HUSSEIN MWINYI; ZANZIBAR MUACHE TABIA YA MUHALI

    Bisaya Raphael May 31, 2021 Habari
    Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameitaka jamii ya Wazanzibari kuacha tabia ya ''muhali'' na kuripoti matukio ya vitendo vya udhalilishaji katika vyombo vya sheria huku akilitaka jeshi la Polisi kuacha kufanya usuluhishi wa matukio hayo.
     
    Akizungumza na wananchi pamoja na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wa Mkoa wa Mjini Kichama  hapo Makao Makuu ya Chama hicho Mkoa Amani, katika ziara ya kuwashukuru, alisema bado hajaridhishwa na utendaji wa jeshi la Polisi katika kushughulikia kesi za udhalilishaji wa kijinsia.
     
    Rais Dk. Mwinyi ambaye pia, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) alisema yapo malalamiko kutoka kwa jamii kwamba jeshi la Polisi limekuwa likifanya upatanishi wa kusuluhisha wa kesi hizo katika vituo vya Polisi na kumalizana kienyeji.
     
    Alifahamisha hizo sio kazi za jeshi la Polisi kwa mujibu wa sheria  ambapo wanatakiwa kuhakikisha wanatayarisha kesi kwa kufanya upelelezi na kuzipeleka mbele kwa hatua nyengine.
     
    Hivyo, Rais Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kuwapongeza Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa kufanya marekebisho mazuri katika sheria za udhalilishaji ambapo mtuhumiwa wa makosa hayo atakuwa akinyimwa  dhamana.

    Related Posts

    Habari

    Post a Comment

    No comments

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    KWA SHEREHE NA SEMINA KARIBU UKUMBI WA LAKE TANGANYIKA, NZEGA-TABORA

    FOOTBALL STORIES

    Follow us

    • Like on Facebook
    • Follow on Twitter
    • Follow on Instagram
    • Subscribe on Youtube

    Popular Posts

    • Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      *https://youtu.be/-P4s8sVq31o* 🤔🤔🤔🤔🤔 *JE NI HALALI KWA MKRISTO KULIPA MAHARI ILI AOE?????* 🤔🤔🤔🤔🤔 . . . Hebu tutazame k...
    • kusuka na unyoaji katika Biblia
      kusuka na unyoaji katika Biblia
       KAMA MUNGU ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAWAKE ! NDIVYO ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAUME PIA. BWANA YESU asifiwe!😅 Maranatha!😅🙏🏻 N...
    • HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      KANISA LA #SDA LINA MISINGI 28 AMBAYO NI 1.Neno la Mungu 2.Utatu mtakatifu 3.Mungu baba 4.Mungu mwana 5.Roho mtakatifu 6.Uumbaji...

    Labels

    Habari MICHEZO Live injili Tamthilia Kesha la Asubuhi BREAKING NEWS magazeti Matangazo Covid19 Mastaa Viongozi today's quote Lesoni leo Wimbo wa Leo barikiwa Je Wajua? KULFI Bongo Movies Stories TETESI ZA USAJILI

    Facebook

    Created By SoraTemplates | Distributed By Gooyaabi Templates