• HOME
  • BREAKING NEWS
  • TAMTHILIA
  • MICHEZO
  • MATANGAZO
  • CONTACT US

BINAGO BLOG

  • Home
  • Home / Habari / WAKAZI WA NSIMBO WALIA NA HALI TETE YA USALAMA

    WAKAZI WA NSIMBO WALIA NA HALI TETE YA USALAMA

    Bisaya Raphael October 08, 2021 Habari
    Wananchi wa Kata ya Kanoge Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wameiomba Serikali kuingilia ili kukomesha matukio ya unyanyasaji vikiwemo vipigo, wanayofanyiwa na Viongozi wao wa Kata.

    Hii ni kufuatia matukio ya mara kwa mara ya kupigwa kwa wananchi yanayowahusisha viongozi wa kata hiyo.

    Katika tukio la hivi karibuni kabisa limetokea Oktoba 7, 2021 likimhusisha mwanaume mmoja aliyetambuliwa kwa majina ya Erneste Melkiore (45) aliyepigwa na watu wawili wanaodaiwa kuwa ni walinzi wa majengo ya iliyokuwa shule ya msingi Nsanda.

    Katika tukio hilo Melkiore anadai kuvamiwa na watu hao wakati akisafisha shamba lake lililopo jirani na majengo hayo na kisha kupigwa sehemu mbalimbali kabla ya kufungwa miguu na mikono kisha kufungwa nyuma ya pikipiki na kuburuzwa kwa umbali wa zaidi ya mita 200.

    "Walinifunga kamba miguu na mikono, wakaniburuza umbali wa viwanja viwili vya mpira, baadae wakaanza kunipiga wakidai wanataka kunilainisha" alisema Melkiore

    Aidha baada ya kichapo hicho Melkiore alitelekezwa kituo cha polisi Kanoge bila kuchukuliwa maelezo wala huduma yoyote mpaka alipochukuliwa ndugu zake na kukimbizwa katika kituo cha Afya Kanoge akiwa katika hali mbaya.

    "Baada ya kunipiga walinipeleka kituo cha polisi, walidai wao ni walinzi wa msitu, askari aliwapigia simu watu wa maliasili (TFS) wakadai wao hawajawatuma na hawawatambui" alisema Melkiore

    Katika tukio lingine linalofanana na hilo linamhusisha Joseph Bamila (60) lililotokea Agosti 15, 2021 baada ya mzee huyu kuchukuliwa nyumbani kwake usiku kupelekwa ofisi za kata na Afisa mtendaji wa Kata ya Nsimbo kwa kushirikiana na Afisa Maendeleo wa Kata hiyo na kisha kupokea kipigo cha nguvu kilichomuachia kilema cha maisha.

    Akielezea tukio hilo mzee Bamila amesema mpaka sasa haelewi sababu hasa ya yeye kufanyiwa unyama ule kwani hajawahi kushtakiwa kuhusiana na tukio hilo na hata waliomfanyia kitendo kile hawajashtakiwa licha ya yeye kulalamika.

    Kufuatia matukio hayo wananchi wa kata hiyo wanadai kutokuwa na imani na serikali ya kata hiyo kwani katika matukio yote mawili na mengine yanayotokea viongozi wa serikali wamekuwa wakijitenga nayo.

    Related Posts

    Habari

    Post a Comment

    No comments

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    KWA SHEREHE NA SEMINA KARIBU UKUMBI WA LAKE TANGANYIKA, NZEGA-TABORA

    FOOTBALL STORIES

    Follow us

    • Like on Facebook
    • Follow on Twitter
    • Follow on Instagram
    • Subscribe on Youtube

    Popular Posts

    • kusuka na unyoaji katika Biblia
      kusuka na unyoaji katika Biblia
       KAMA MUNGU ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAWAKE ! NDIVYO ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAUME PIA. BWANA YESU asifiwe!😅 Maranatha!😅🙏🏻 N...
    • Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      *https://youtu.be/-P4s8sVq31o* 🤔🤔🤔🤔🤔 *JE NI HALALI KWA MKRISTO KULIPA MAHARI ILI AOE?????* 🤔🤔🤔🤔🤔 . . . Hebu tutazame k...
    • HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      KANISA LA #SDA LINA MISINGI 28 AMBAYO NI 1.Neno la Mungu 2.Utatu mtakatifu 3.Mungu baba 4.Mungu mwana 5.Roho mtakatifu 6.Uumbaji...

    Labels

    Habari MICHEZO Live injili Tamthilia Kesha la Asubuhi BREAKING NEWS magazeti Matangazo Covid19 Mastaa Viongozi today's quote Lesoni leo Wimbo wa Leo barikiwa Je Wajua? KULFI Bongo Movies Stories TETESI ZA USAJILI

    Facebook

    Created By SoraTemplates | Distributed By Gooyaabi Templates