AMKA NA BWANA LEO 17
*KESHA LA ASUBUHI.*
Jumanne, 17/08/2021.
*ISHI NA ROHO YA FURAHA,*
*Maana nadhani ya kuwa Mungu ametutoa sisi mitume mwisho, kama watu waliohukumiwa wauawe; kwa sababu tumekuwa tamasha kwa dunia; kwa malaika na wanadamu. 1 Wakorintho 4:9.*
▶️Bwana ni mwema na anayestahili kusifiwa sana. Hebu na tujifunze kumsifu kwa sauti zetu, na kutambua kwamba wakati wote tuko katika ushirika mzuri kabisa-pamoja na Mungu na pamoja na Mwanawe, Yesu. Sisi ni tamasha kwa ulimwengu ambao haukuanguka, kwa malaika, na kwa wanadamu wenzetu. Kulitambua hili kutatuongoza kusonga mbele kadiri Bwana atakavyoelekeza, kwa moyo thabiti, uliopangwa vizuri.
▶️Hebu na tukeshe na kuomba. Hii itatusaidia kutambua kwamba tunapaswa kuwa chini ya mamlaka ya kuongozwa na Kristo, Kiongozi wetu wa kiungu. Yeye hutupatia uthabiti wa kusudi, na mihemko iliyodhibitiwa, kama ya Kristo, na busara, vinavyotuwezesha kuwaza kwa utulivu, na kwa wema. Muda kwa juma ni mfupi sana kwetu kujinyima furaha. Tutapaswa, ndugu na dada yangu mpendwa, kujenga roho ya furaha, kwa sababu tunajua kwamba tunaye Mwokozi anayetupenda, na ambaye atatubariki ikiwa tutakaribisha uwapo Wake mioyoni mwetu.
▶️Hatuwezi kuthubutu kutumia talanta ya kusema kwa namna ambayo haitamnufaisha mtu yeyote. Neno la Mungu linarekebisha chanzo cha hisi na matendo yetu kila mmoja kwa mwenzake, hali ya moyo hurekebisha kanuni za maisha ya ndani. Kanuni safi, ambazo hazijaghushiwa zitachochea maneno na matendo sahihi. Vipaji vyetu ni lazima viongezeke, vinginevyo vitapungua.
▶️Tunapaswa kuwa watoto wadogo wa Kristo, tukijifunza kutoka kwake. Tunapaswa kwa ukamilifu kuamini na kutekeleza ukweli tunaoukiri—kwamba mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kila wakati lazima tuwe tayari kushuhudia kujitokeza kwa matukio ya ajabu. Kila siku tunapaswa kuweka wakfu upya maisha yetu kwa ajili ya huduma ya Bwana, na kufungua mlango wa moyo kumkaribisha Mgeni wa mbinguni na kupokea upendo wake.
▶️Katika wakati wa usiku nimekuwa nikiomba sana kwa ajili ya utambu
Post a Comment