• HOME
  • BREAKING NEWS
  • TAMTHILIA
  • MICHEZO
  • MATANGAZO
  • CONTACT US

BINAGO BLOG

  • Home
  • Home / Habari / WATAKIWA KUFANYA KAZI BILA KUCHAFUA MAZINGIRA

    WATAKIWA KUFANYA KAZI BILA KUCHAFUA MAZINGIRA

    Bisaya Raphael June 12, 2021 Habari
    Waziri  wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe.Selemani Jafo amesema kuwa Taifa linahitaji uwekezaji wa Viwanda ambavyo vinalinda na kuhifadhi mazingira yetu kwa manufaa ya Kizazi kilichopo na kijacho.

    Jafo alisema hayo mjini Kibaha mkoani Pwani alipofanya ziara katika kiwanda cha Vunjo Afro Company kinachozalisha misumari kilichopo eneo la Misugusugu alipofanya ziara kujionea hali ya kimazingira.

    Alibaini changamoto mbalimbali za kimazingira pamoja na kubadilisha jina la kiwanda bila kutoa taarifa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).

    Aidha, waziri huyo aliwataka wenye kiwanda hicho kufanya uzalishaji bila ya kuchafua mazingira kwani Serikali inataka maisha bora kwa wananchi wenye afya bora na salama.

    Alionesha kutoridhishwa na mazingira ya kiwanda ambapo ameahidi kutokifunga na amekipa wiki mbili kuhakikisha maji yanayotumika wakati wa uzalishaji hayatiririshwi kwenda kwenye mazingira.

    Pia aliwataka watoe taarifa juu ya utupaji wa uchafu au vumbi linalobaki kutoka kwenye chuma baada ya kuzalisha.

    “Vumbi litokanalo na chuma ni hatari kwa maisha ya binadamu na viumbe hai, ikiwa kama kiwanda mnashindwa kueleza kuwa hili vumbi mnalipeleka wapi basi kwa asilimia kubwa ni wachafuzi wa mazingira yetu na hamna huruma na wananchi juu ya Maisha yao bali mnaangalia masilahi yenu.

    "Kutokana na kushindwa kujieleza vizuri natoa wiki mbili kwenu mnieleze wapi mnapeleka vumbi hili, niseme tu kweli sijaridhika na mazingira na mwenendo wa kiwanda hiki, tunataka uwekezaji lakini uwekezaji wenye tija kwa Taifa, hivyo NEMC hakikisha mnafanya ukaguzi na kutoa maelekezo kwa kiwanda hiki," alisema Waziri Jafo.

    Related Posts

    Habari

    Post a Comment

    No comments

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    KWA SHEREHE NA SEMINA KARIBU UKUMBI WA LAKE TANGANYIKA, NZEGA-TABORA

    FOOTBALL STORIES

    Follow us

    • Like on Facebook
    • Follow on Twitter
    • Follow on Instagram
    • Subscribe on Youtube

    Popular Posts

    • kusuka na unyoaji katika Biblia
      kusuka na unyoaji katika Biblia
       KAMA MUNGU ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAWAKE ! NDIVYO ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAUME PIA. BWANA YESU asifiwe!😅 Maranatha!😅🙏🏻 N...
    • Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      *https://youtu.be/-P4s8sVq31o* 🤔🤔🤔🤔🤔 *JE NI HALALI KWA MKRISTO KULIPA MAHARI ILI AOE?????* 🤔🤔🤔🤔🤔 . . . Hebu tutazame k...
    • HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      KANISA LA #SDA LINA MISINGI 28 AMBAYO NI 1.Neno la Mungu 2.Utatu mtakatifu 3.Mungu baba 4.Mungu mwana 5.Roho mtakatifu 6.Uumbaji...

    Labels

    Habari MICHEZO Live injili Tamthilia Kesha la Asubuhi BREAKING NEWS magazeti Matangazo Covid19 Mastaa Viongozi today's quote Lesoni leo Wimbo wa Leo barikiwa Je Wajua? KULFI Bongo Movies Stories TETESI ZA USAJILI

    Facebook

    Created By SoraTemplates | Distributed By Gooyaabi Templates