UTEKELEZAJI WA BAJETI WA MWAKA 2020/21
Waziri Bashungwa amesema matumizi ya Kiswahili yanaongezeka kwa kasi duniani, kuongeza kukubalika kwa lugha hiyo kunachagizwa na msukumo wa kustawisha lugha hiyo unaoendelea kufanywa na unaoendelea kufanywa na viongozi wa kitaifa akiwemo Rais wa Awamu ya Sita Mhe. Samia Suluhu Hassan, aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na watangulizi wao.
Amesisitiza kuwa Wizara yake iliendesha kongamano Mei 21, 2021 ambalo lilizinduliwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kwa lengo la kutambua na kuenzi mchango wa Tanzania katika Harakati za Ukombozi wa nchi za Afrika ili kutangaza, kuhamasisha, na kuelimisha jamii kuhusu urithi wa ukombozi wa Bara la Afrika uliopo nchini.
“Mwaka 2011 Tanzania ilikabidhiwa na Umoja wa Afrika (AU) jukumu la kuratibu Programu ya Afrika ya “Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika ambayo ilipewa jukumu la kukusanya, kuhifadhi na kutangaza kumbukumbu kuhusu harakati za Ukombozi wa Bara la Afrika ikiwemo nyaraka, makaburi, majengo, mahandaki, silaha, sare, hotuba na magari kwa matumizi ya vizazi vya sasa na vijavyo ambayo makao yake makuu yapo Jijini Dar es Salaam” amesema Mhe. Bashungwa.
Katika sekta ya Maendeleo ya Sanaa, Wizara imefanikiwa kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma kwa wasanii na wadau wa sanaa ambapo Taasisi zinazowahudumia Wasanii za BASATA, Bodi ya Filamu na COSOTA zimewekwa katika eneo moja kwenye jengo la UTUMISHI lililopo Kivukoni. Hatua hii pamoja na mambo mengine, itawapunguzia muda, kadhia na gharama wasanii wetu na wadau wengine wanaohudumiwa na Taasisi hizi.
Timu za mpira wa miguu nchini zinaendelea kufanya vizuri ikiwemo Timu ya Tanzanite ya Wanawake wenye umri chini ya miaka 17 imefanikiwa kutwaa Kombe la COSAFA baada ya kuzifunga timu kutoka Comoro, Afrika Kusini, Zimbwabwe na Zambia nchini Afrika Kusini mwezi Novemba, 2020 wakati mchezo wa ngumi mabondia Hassan Mwakinyo, Ibrahim Class, Salim Jengo, Tony Rashid, Bruno Tarimo.
Post a Comment