• HOME
  • BREAKING NEWS
  • TAMTHILIA
  • MICHEZO
  • MATANGAZO
  • CONTACT US

BINAGO BLOG

  • Home
  • Home / Habari / UMITASHUMTA, UMISSETA KUFUNGULIWA MTWARA

    UMITASHUMTA, UMISSETA KUFUNGULIWA MTWARA

    Bisaya Raphael June 02, 2021 Habari
    Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, anatarajiwa kufungua Mashindano ya Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi (UMITASHUMTA) na Sekondari (UMISSETA) Juni 8, 2021 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

    Akitoa taarifa kwa umma, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe amesema mashindano ya UMITASHUMTA yafanyika Juni 6-19, 2021 ambapo UMISSETA yataanza Juni 19 hadi Julai 3, 2021.

    "Jumla ya washiriki wapatao 3,600 kutoka Mikoa yote Tanzania Bara wanatarajiwa kushiriki katika michezo ya UMITASHUMTA na washiriki 3,800 kutoka Mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar watashiriki katika michezo ya UMISSETA," amesema Prof. Shemdoe.

    Aidha, Katibu Mkuu huyo ameitaja michezo itakayohusika kuwa mpira wa miguu, netiboli, mpira wa wavu, mpira wa mikono, mpira wa meza, riadha jumuishi, kwaya na ngoma. Aidha, mchezo wa mpira wa kikapu utahusisha shule za Sekondari kwa wavulana na wasichana.

    Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. James Mdoe, amesema michezo inajenga afya, ubunifu, upendo, hali ya kujiamini na umoja wa kitaifa.

    "Serikali imekwisha elekeza kuendelea na uimarishaji wa ufundishaji wa michezo shuleni sambamba na kuendeleza na kuimarisha mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA katika ngazi zote ikiwemo hii ya Taifa," ameeleza.

    Naye Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi amesema viongozi wa mashirikisho na vyama vya michezo ili wajionee vipaji na kwamba mashindano hayo yatarushwa mubashara kupitia TV mbalimbali nchini.

    "Tutaendelea kuboresha michezo hii ili iwe kitovu cha kuandaa, kukuza na kuuza vipaji vya vijana wetu," amedokeza Dkt. Abbasi.

    Aidha, amesema zaidi ya wachezaji 26 hivi sasa katika ligi kuu na ligi ya daraja la kwanza wametokana na mashindano hayo huku ikitoa takriban asilimia 95 ya wachezaji wa timu za soka za vijana.

    Related Posts

    Habari

    Post a Comment

    No comments

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    KWA SHEREHE NA SEMINA KARIBU UKUMBI WA LAKE TANGANYIKA, NZEGA-TABORA

    FOOTBALL STORIES

    Follow us

    • Like on Facebook
    • Follow on Twitter
    • Follow on Instagram
    • Subscribe on Youtube

    Popular Posts

    • kusuka na unyoaji katika Biblia
      kusuka na unyoaji katika Biblia
       KAMA MUNGU ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAWAKE ! NDIVYO ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAUME PIA. BWANA YESU asifiwe!😅 Maranatha!😅🙏🏻 N...
    • Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      *https://youtu.be/-P4s8sVq31o* 🤔🤔🤔🤔🤔 *JE NI HALALI KWA MKRISTO KULIPA MAHARI ILI AOE?????* 🤔🤔🤔🤔🤔 . . . Hebu tutazame k...
    • HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      KANISA LA #SDA LINA MISINGI 28 AMBAYO NI 1.Neno la Mungu 2.Utatu mtakatifu 3.Mungu baba 4.Mungu mwana 5.Roho mtakatifu 6.Uumbaji...

    Labels

    Habari MICHEZO Live injili Tamthilia Kesha la Asubuhi BREAKING NEWS magazeti Matangazo Covid19 Mastaa Viongozi today's quote Lesoni leo Wimbo wa Leo barikiwa Je Wajua? KULFI Bongo Movies Stories TETESI ZA USAJILI

    Facebook

    Created By SoraTemplates | Distributed By Gooyaabi Templates