• HOME
  • BREAKING NEWS
  • TAMTHILIA
  • MICHEZO
  • MATANGAZO
  • CONTACT US

BINAGO BLOG

  • Home
  • Home / BREAKING NEWS / Habari / DKT. ZAINAB CHAULA AFUNGUA MAFUNZO KWA WANAWAKE

    DKT. ZAINAB CHAULA AFUNGUA MAFUNZO KWA WANAWAKE

    Bisaya Raphael May 11, 2021 BREAKING NEWS, Habari
    Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Zainab Chaula amefungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wasichana na wanawake ili waweze kushiriki kikamilifu katika masuala ya ubunifu katika sekta mbalimbali ambapo kwa namna moja ama nyingine watatumia TEHAMA katika kufanya tafiti zao na kutafuta masoko ya kuuza na kununua bidhaa zao.

    Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dodoma Dkt. Chaula ametoa rai kwa waandaaji wa mafunzo hayo kuongeza wigo wa washiriki hasa wanaohusika na kutoa maamuzi kwa kuwa Serikali imejipanga kutambua, kuwezesha na kuendeleza ubunifu na teknolojia zinazozalishwa nchini ambapo hadi sasa ushiriki wa watoto wa kike na wanawake bado ni mdogo sana.

    “Ubunifu ni namna mtu anakuja na jambo lake jipya, analiunda mwenyewe, analitengeneza mwenyewe, analisimamia mwenyewe kulingana na fikra zake ndio maana hapa leo tupo na Ndoto Hub kila mtu anaishi kulingana na fikra na ndoto zake, anatamani afikie sehemu fulani na kuwashawishi wengine ili nao wapate ndoto kupitia wengine”, alizungumza Dkt. Chaula

    Ameongeza kuwa ni muhimu dhana nzima ya ubunifu kueleweka kwa jamii sambamba na kuangazia madhara ya kutohusisha mwanamke na mtoto wa kike katika masuala ya ubunifu na madhara ya kutokuendeleza ubunifu ulioletwa na wabunifu katika maeneo mbalimbali ya kisekta ili Serikali iweze kufanyia kazi maeneo ambayo yataainishwa.

    Akizungumza katika mafunzo hayo Mbunge wa viti maalum CCM kutoka katika kundi la Asasi za Kiraia Tanzania Bara Mhe. Neema Lugangira amesema kuwa wapo katika mafunzo hayo kujadili kwa pamoja na kuona namna ambayo mwanawake na mtoto wa kike wanaweza kushiriki katika masuala ya ubunifu na teknolojia kwa kuziangazia changamoto zinazowakwamisha na kuzitafutia ufumbuzi.

    Related Posts

    Habari

    Post a Comment

    No comments

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    KWA SHEREHE NA SEMINA KARIBU UKUMBI WA LAKE TANGANYIKA, NZEGA-TABORA

    FOOTBALL STORIES

    Follow us

    • Like on Facebook
    • Follow on Twitter
    • Follow on Instagram
    • Subscribe on Youtube

    Popular Posts

    • kusuka na unyoaji katika Biblia
      kusuka na unyoaji katika Biblia
       KAMA MUNGU ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAWAKE ! NDIVYO ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAUME PIA. BWANA YESU asifiwe!😅 Maranatha!😅🙏🏻 N...
    • Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      *https://youtu.be/-P4s8sVq31o* 🤔🤔🤔🤔🤔 *JE NI HALALI KWA MKRISTO KULIPA MAHARI ILI AOE?????* 🤔🤔🤔🤔🤔 . . . Hebu tutazame k...
    • HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      KANISA LA #SDA LINA MISINGI 28 AMBAYO NI 1.Neno la Mungu 2.Utatu mtakatifu 3.Mungu baba 4.Mungu mwana 5.Roho mtakatifu 6.Uumbaji...

    Labels

    Habari MICHEZO Live injili Tamthilia Kesha la Asubuhi BREAKING NEWS magazeti Matangazo Covid19 Mastaa Viongozi today's quote Lesoni leo Wimbo wa Leo barikiwa Je Wajua? KULFI Bongo Movies Stories TETESI ZA USAJILI

    Facebook

    Created By SoraTemplates | Distributed By Gooyaabi Templates