AMKA NA BWANA LEO 12

KESHA LA ASUBUHI

Jumatano 12/05/2021

*OMBA, AMINI, DAI*

*Midomo ya uongo ni chukizo kwa BWANA; Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.* *Mithali 12:22*

Nina kazi ya kufanya na kwa neema ya Kristo nitaifanya. Wasiwasi wangu mkubwa ni kwa wale ambao ni rahisi sana kuuamini uongo kuliko kuuamini ukweli. Je, nitawafanyia nini hawa? Ninaweza kufanya jambo gani ili niwaokoe ili wasiseme uongo, wala wasiupende uongo baada ya kuwa wameusema? Kitu ninachoweza kufanya ni kumwasilisha Kristo, Mwokozi wa thamani awe mfano kwao. 

*Kama wanampenda Yesu watakuwa safi, wasio na mawaa, wasionajisi.Watazungukwa na angahewa ya imani badala ya mashaka na kusitasita na kutokuamini. Watazungumza kuhusu Yesu, kuhusu mbinguni, kuhusu wajibu wa Mkristo, pambano la Mkristo, na jinsi ya kufanikiwa kuzishinda nguvu za Shetani.* Hawatakuwa kama wanyama wala mizoga wakishambulia yale yanayoonekana kuwa madhaifu ya wengine. 

Naam, ili Yesu aweze kufunuliwa kwao! Naam, ili waweze kupenda kukaa katika upendo Wake usio na kifani! Naam, ili mioyo yao ijifunze pamoja na upendo Wake, kisha tusikae bila kujua mbinu za Shetani. Silaha zetu zinaweza kugeuzwa dhidi ya maadui zetu hatari zaidi. Kwa imani tunapaswa kuona kwa nuru halisi; macho ya malaika wa mbinguni yameelekezwa kwetu kwa makusudi kwa upendo ili kuona kujitoa kwetu. Kwa imani tunapaswa kumwona Shetani akifuatilia kuona kila kosa—kila kitu ambacho anaweza kutumia dhidi yetu, akitumia fursa ya sisi kutokuwa na umoja na upendo, akifanya udanganyifu na akishangilia ushindi anawashitaki hawa mbele ya malaika wa Mungu.

*Kwa sababu hatuna uwezo wa kushindana na dhambi na Shetani, basi tumepewa usaidizi. Omba nawe utapokea. Wawili au watatu wanaweza kuidai ahadi hii, ikiwa wataomba kitu chochote kwa jina Lake, atafanya*. Ataombwa kufanya mambo haya kwa ajili yetu. 

Mpendwa ndugu yangu, usijihisi unajitegemea sana kwamba hutaweza kuomba msaada wa Yule pekee ambaye anaweza kukupatia usaidizi unaohitaji kuvunja mtego wa Shetani. *Unapaswa kuwa mwangalifu, mwenye ari, mwaminifu na mkweli; mnyenyekevu na wa kuaminika, uliyejawa upole na huruma.*

 *lanze kazi moyoni mwako, kisha, moyo wako ukiwa umebatizwa kwa Roho wa Kristo, waongoze watoto wako kwa Mwanakondoo wa Mungu.*

*MUNGU ATUBARIKI TUNAPOTAFAKARI NENO LAKE*

No comments