WANAWAKE WATAKIWA KUWAPA WANAUME ZAO TENDO LA NDOA

Mwenyekiti wa Kituo cha Taarifa na Maarifa kata ya Shilela kinachosimamiwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Bi. Rahabu Nkwabi amewataka akina mama kuwapatia haki ya ndoa waume zao na kuepuka visingizio na sababu za mara kwa mara kuwa hawawezi kushiriki tendo la ndoa kwani kitendo cha kunyimana tendo la ndoa kinasababisha migogoro hali inayopelekea kupigana ndoa kuvunjika na kusababisha watoto kuteseka, kutelekezwa na kuacha shule,kuolewa wangali wadogo au kuzurura tu mtaani.

“Wanawake wapeni tendo la ndoa waume zenu, acheni visingizio. Mkiwanyima ndiyo maana wengine wanaamua kuanza kuchepuka matokeo yake

Kwa upande mwingine akasema matukio ya ukatili wa kijinsia katika familia nyingi yamekuwa yakisababishwa na tabia za wanandoa kuanza kusaliti wenza wao matokeo yake wanashindwa kupatiana haki ya ndoa hali inayosababisha wanandoa hao kuanza kuchepuka ili kukidhi haja zao za kimwili.

“Wanawake vunjeni ukimya, fungukeni kuhusu akina baba wanaolala na suruali kwani wanawafanyia ukatili wa kingono kwa kuwanyima haki yenu ya ndoa,” amesema Rahabu.

“Mwanaume kwanini ulale na mke wako huku umevaa suruali? ulioa kwa ajili ya nini,huoni kuwa unamnyima haki yake mkeo na kumfanya awaze kuwa unamsaliti kwa kufanya ngono na wanawake wengine nje ya ndoa. Kwanini ulale na suruali wakati mwenzako anataka.

No comments