• HOME
  • BREAKING NEWS
  • TAMTHILIA
  • MICHEZO
  • MATANGAZO
  • CONTACT US

BINAGO BLOG

  • Home
  • Home / Habari / WAHAMIAJI 9 WA BURUNDI WATIWA MBARONI MKOANI SHINYANGA

    WAHAMIAJI 9 WA BURUNDI WATIWA MBARONI MKOANI SHINYANGA

    Bisaya Raphael August 03, 2021 Habari
    Afisa Uhamiaji Mkoa wa Shinyanga Naibu Kamishna (DCI) Rashid Magetta amethibitisha kukamatwa kwa wahamiaji hao ikiwa ni matokeo ya oparesheni inayoendelea Mkoani humo dhidi ya wahamiaji haramu.

    Jumla ya raia 9 wa Burundi wamekamatwa Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga, wakiwa wamepangiwa nyumba na mtanzania ambaye alikuwa anawatumikisha ktk kazi za vibarua hususani kuchunga ng'ombe na kuandaa mashamba ya tumbaku.

    Pamoja na Warundi hao mwenyeji wao raia wa Tanzania na ndugu zake wawili pia wamekamatwa na kesho wote watafikishwa mahakamani, kujibu mashtaka ya kuingia na kuishi nchini kinyume cha sheria sambamba na makosa ya raia wa Tanzania kuhifadhi na kuwatumikisha wahamiaji hao.

    DCI Magetta amewataka wananchi mkoani humo kuacha kabisa vitendo vya kusafirisha na kuhifadhi wahamiaji haramu kwani vitendo hivyo ni kosa kwa mujibu wa sheria ya Uhamiaji sura 54 Rejeo la mwaka 2016 pamoja na kanuni zake ambapo watuhumiwa wakithibitika kutenda makosa hayo adhabu yake ni kifungo cha miaka ishirini (20) au kulipa faini isiyopungua shilingi milioni ishirini (20) au vyote kwa pamoja.

    Related Posts

    Habari

    Post a Comment

    No comments

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    KWA SHEREHE NA SEMINA KARIBU UKUMBI WA LAKE TANGANYIKA, NZEGA-TABORA

    FOOTBALL STORIES

    Follow us

    • Like on Facebook
    • Follow on Twitter
    • Follow on Instagram
    • Subscribe on Youtube

    Popular Posts

    • kusuka na unyoaji katika Biblia
      kusuka na unyoaji katika Biblia
       KAMA MUNGU ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAWAKE ! NDIVYO ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAUME PIA. BWANA YESU asifiwe!😅 Maranatha!😅🙏🏻 N...
    • Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      *https://youtu.be/-P4s8sVq31o* 🤔🤔🤔🤔🤔 *JE NI HALALI KWA MKRISTO KULIPA MAHARI ILI AOE?????* 🤔🤔🤔🤔🤔 . . . Hebu tutazame k...
    • HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      KANISA LA #SDA LINA MISINGI 28 AMBAYO NI 1.Neno la Mungu 2.Utatu mtakatifu 3.Mungu baba 4.Mungu mwana 5.Roho mtakatifu 6.Uumbaji...

    Labels

    Habari MICHEZO Live injili Tamthilia Kesha la Asubuhi BREAKING NEWS magazeti Matangazo Covid19 Mastaa Viongozi today's quote Lesoni leo Wimbo wa Leo barikiwa Je Wajua? KULFI Bongo Movies Stories TETESI ZA USAJILI

    Facebook

    Created By SoraTemplates | Distributed By Gooyaabi Templates