Advertisement

Responsive Advertisement

UCHUMI WA KOREA KASKAZINI WAZIDI KUIMARIKA

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amesema uchumi wa nchi hiyo umeimarika mwaka huu lakini ametaka hatua za kukabiliana na hali ya chakula "ya wasiwasi" inayosababishwa na janga la coronavirus na vimbunga vya mwaka jana.

Kim aliongoza mkutano wa jumla wa kamati kuu ya Chama tawala cha Wafanyakazi Jumanne kukagua maendeleo juu ya sera kuu na hatua za ufundi kusuluhisha maswala ya kiuchumi, kulingana na shirika rasmi la habari la KCNA.

Kamati iliweka malengo na majukumu kufanikisha mpango wake mpya wa uchumi wa miaka mitano ulioainishwa katika kikao chake cha awali mnamo Februari, pamoja na kuongezeka kwa uzalishaji wa chakula.

Kim alisema uchumi wa jumla umeboreshwa katika nusu ya kwanza ya mwaka, na jumla ya pato la viwanda liliongezeka kwa 25% kutoka mwaka mmoja uliopita, KCNA ilisema.

"Lakini kulikuwa na "mfululizo wa kupotoka" katika juhudi za chama kutekeleza mipango hiyo kwa sababu ya vizuizi kadhaa"

"Hali ya chakula ya watu sasa inazidi kuwa mbaya wakati sekta ya kilimo ilishindwa kutimiza mpango wake wa uzalishaji wa nafaka kutokana na uharibifu wa kimbunga mwaka jana," Kim alisema.

Post a Comment

0 Comments