Mwambe ametoa taarifa hiyo leo Ijumaa Aprili 20, 2018 bungeni mjini Dodoma wakati Mchungaji Getrude akitoa maoni yake kuhusu bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto mwaka 2018/19.
“Mheshimiwa Spika napenda kujua kama kanisa la mama Rwakatare kuna maombi ya kuponya watu ukimwi ili kuweza kuisaidia Serikali,” amesema Mwambe.
Baada ya taarifa hiyo Mchungaji Rwakatare amesema, “Mambo hayo yapo wewe walete tu.”
