➪Baada ya kufanikiwa kutinga robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika kwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya USGN juzi, kikosi cha Simba kilirejea kambini jana jioni kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union
➪Keshokutwa Alhamisi, mabingwa watakuwa mkoani Tanga uwanja wa Mkwakwani kuikabili Coastal Union
➪Baada ya mchezo huo, Simba itaelekea Arusha ambako wanakabiliwa na mchezo mwingine wa ligi kuu ambao ni wa kiporo dhidi ya Polisi Tanzania
➪Kocha Mkuu wa Simba Pablo Franco aliwapa wachezaji mapumziko ya siku moja baada ya mchezo dhidi ya USGN
0 Comments