Advertisement

Responsive Advertisement

KLABU YA SIMBA SC KUKABIDHIWA KOMBE LAO LA VPL LEO

Kama Bodi  ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) ilivyotangaza kuwa leo Julai 18, 2021 ndio siku maalum ya kukabidhi rasmi Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom 2020/2021 kwa klabu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam.

Simba ambao walitwaa ubingwa huo Julai 11 baada ya kufikisha alama 79 kufuatia ushindi wa mabao 2-0 walioupata dhidi ya Coastal Union FC, muda huu wanakabidhiwa Kombe hilo na Medali baada ya kumalizika kwa mchezo wao wa mwisho wa Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya Namungo FC.

Post a Comment

0 Comments