MAKAO MAKUU YA FITI KUHAMISHIWA MAFINGA

Waziri ya Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbari amesema Wizara ya Maliasili na Utalii iko katika mchakato wa kukihamisha chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) kilichopo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro kuhamia Mafinga mkoani Iringa, ili kukiwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi kutokana na uwepo malighafi za misitu katika eneo hilo.

Ameyasema hayo wakati alipotembelea chuo hicho na kuzungumza na uongozi, na kuongeza kuwa kutokana na uwepo wa misitu huko Mafinga hakutakuwa na haja ya kutumia gharama za kusafirisha magogo kwa ajili ya matumizi ya kutengeneza bidhaa mbalimbali zitokanazo na misitu chuoni hapo.

“Mafinga ndio sehemu yenye viwanda vingi vya mbao vya watu binafsi, na hiyo itasaidia Wanafunzi kufanya mafunzo kwa vitendo katika viwanda hivyo na tunazo hekta 120 za Serikali ambazo sio za kununua na kwamba suala la kuhama haliepukiki.” amesema Waziri Ndumbaro

Amebainisha kuwa chuo cha FITI Moshi hakitafungwa bali kitakuwa ni tawi na kwamba hakitahamishwa

No comments