BARABARA MPYA YA MWANDIGA HADI MWAMGONGO

Muonekano wa sehemu ya uanzishwaji wa barabara mpya ya Mwandiga hadi Mwamgongo mkoani Kigoma inayokadiriwa kuwa na urefu wa kilometa 65 baada ya kukamilika kwake.

Imeelezwa kuwa Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya Mwandiga- Chankere - Mwamgongo (Km 65) kwa kiwango cha changarawe ili kurahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa jimbo la Kigoma Kaskazini na mikoa jirani kwa ujumla.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, wakati wa ziara yake mkoani Kigoma alipokuwa akikagua barabara hiyo.

No comments