• HOME
  • BREAKING NEWS
  • TAMTHILIA
  • MICHEZO
  • MATANGAZO
  • CONTACT US

BINAGO BLOG

  • Home
  • Home / Habari / DHAHABU ZAENDELEA KUSAFISHWA MWANZA

    DHAHABU ZAENDELEA KUSAFISHWA MWANZA

    Bisaya Raphael May 30, 2021 Habari
    Imeelezwa kuwa tangu kuanzishwa kwa kiwanda cha kusafisha dhahabu cha Mwanza, Precious Metals Refinery, jumla ya kilo 63.179 zimesafishwa kwa ubora wa asilimia 99.99.

    Hayo yameelezwa leo na Mtaalam kutoka katika kiwanda hicho, Deusdedith Magala kwenye ziara ya Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula na Kamishna wa Tume ya Madini, Janeth Lekashingo waliyoifanya katika kiwanda hicho kilichopo Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza.

    Kiwanda hicho kinamilikiwa kwa ubia kati ya Serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO)na mwekezaji kutoka Dubai.

    Mara baada ya kupata maelezo kutoka katika Kiwanda hicho, Profesa Kikula alipongeza utendaji wa kiwanda hicho na kuwataka watendaji wake kuendelea kuchapa kazi kwa bidii.

    Katika hatua nyingine viongozi hao wa Tume wametembelea Ofisi ya Madini na soko la Madini Mwanza ambapo wametoa pongezi kwa watumishi wa Ofisi ya Madini Mwanza kwa kuvuka lengo la makusanyo ya maduhuli kwa asilimia152 katika mwaka wa fedha 2020/2021.

    Related Posts

    Habari

    Post a Comment

    No comments

    Subscribe to: Post Comments ( Atom )

    KWA SHEREHE NA SEMINA KARIBU UKUMBI WA LAKE TANGANYIKA, NZEGA-TABORA

    FOOTBALL STORIES

    Follow us

    • Like on Facebook
    • Follow on Twitter
    • Follow on Instagram
    • Subscribe on Youtube

    Popular Posts

    • Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      Je kutoa Mahari ni sawa ktk biblia?
      *https://youtu.be/-P4s8sVq31o* 🤔🤔🤔🤔🤔 *JE NI HALALI KWA MKRISTO KULIPA MAHARI ILI AOE?????* 🤔🤔🤔🤔🤔 . . . Hebu tutazame k...
    • kusuka na unyoaji katika Biblia
      kusuka na unyoaji katika Biblia
       KAMA MUNGU ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAWAKE ! NDIVYO ALIVYOKWISHA KUWAONYA WANAUME PIA. BWANA YESU asifiwe!😅 Maranatha!😅🙏🏻 N...
    • HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      HII NDIO MISINGI YA KANISA LA WASABATO DUNIANI
      KANISA LA #SDA LINA MISINGI 28 AMBAYO NI 1.Neno la Mungu 2.Utatu mtakatifu 3.Mungu baba 4.Mungu mwana 5.Roho mtakatifu 6.Uumbaji...

    Labels

    Habari MICHEZO Live injili Tamthilia Kesha la Asubuhi BREAKING NEWS magazeti Matangazo Covid19 Mastaa Viongozi today's quote Lesoni leo Wimbo wa Leo barikiwa Je Wajua? KULFI Bongo Movies Stories TETESI ZA USAJILI

    Facebook

    Created By SoraTemplates | Distributed By Gooyaabi Templates