Baada ya kifo cha Rais wa Chad, Idriss Deby, jeshi la nchi hiyo limemteua mtoto wake kushika wadhifa huo, uamuzi ambao sasa unapingwa na wanasiasa wa upinzani.
Deby mwenye umri wa miaka 68, ambaye aliiongoza Chad kwa miaka 30, amefariki baada ya kupigwa risasi wakati akiliongoza jeshi kukabiliana na waasi.
Huku mtoto wake, Mahamat Idriss Deby, akitarajiwa kuongoza kwa miezi 18 iliyobaki kabla ya uchaguzi, wapinzani wamesema nchi hiyo haiendeshwi kwa kurithishana.
0 Comments