Advertisement

Responsive Advertisement

HASSAN BUMBULI: TUNAAMINI AZAM NAO NI WAZURI MECHI ITAKUWA NZURI

"Tunafahamu kwamba Azam ni timu nzuri na ni timu kubwa yenye wachezaji wazuri, na wao huwa ikiwa ni mechi dhidi ya Yanga huwa wanajiandaa vizuri kabisa kuliko wanavyojiandaa na mechi zingine"

"Kwa hiyo tunaamini ni mchezo mzuri kabisa ambao utatoa burudani kwa mashabiki. Lakini sisi Yanga Kama ilivyokuwa kawaida yetu tunajiandaa kwa ajili ya kupata Ushindi dhidi ya hawa ndugu zetu wa Azam FC , tukiamini kwamba Ushindi kutoka kwao utatusaidia kwanza kuwaweka huko nyuma ambayo ni nafasi wanayostahili, pia utatusaidia kusogea huko mbele ambako sisi tunakuhitaji especially kwenye ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara"

"Azam wana pointi zetu 3 na hao wengine wanapointi zetu 3, kwa hiyo sisi tuna pointi zetu 6 muhimu kutoka kwa hao ambao tunafukuzana nao hapo Juu," 

Hassan Bumbuli
-Afisa habari wa Yanga SC

Post a Comment

0 Comments