NDUGAI; TUNATENGENEZA VIJANA AMBAO WANACHEZA POOL TABLE TUU AMBAO WAKIKAA NA SIMU WANAPERUZI TUU, NAFIKIRI TUANGALIE NJIA NYINGINE

• Tunatengeneza vijana wa kucheza Pool table, ambao wakikaa na simu wanaperuzi mitandaoni tu, nafikiri labda tuongeze kodi labda itapunguza hata sijui, hivi tufanye kitu gani ili tuhakikishe kila mtu anafanya kazi, maafisa maendeleo ya jamii hawafanyi kazi  - Ndugai

• Uchumi wa nchi hii umeshikwa na Darasa la 7 ndiyo wanaolima Pamba, Tumbaku na Korosho na ndiyo wanaofuga, ni wasomi wangapi wanafuga? sasa hivi kila anayefaulu anaenda Sekondari na kila anayemaliza form 4, akili yake kwamba mimi nimeondokana na kilimo - Spika Ndugai

• Kwanini kila Mama anataka 'housegirl' atoke Iringa na siyo Dodoma, kwanini siyo mabinti wa Kigogo? ni mabinti wa Kihehe, Iringa ni wachapakazi unaweza ukasema viwanda, huku kwenye kuzalisha yupo nani? elimu yetu inawafanya hawa wapende hivi vitu vya kuzalisha? - Ndugai

• Mnasema sijui tuzalishe nini, hebu lima hekari 1000 za Mahindi fanya kila kazi nani atavuna? kuna form 4 hata mmoja atakuja kukusaidia kuvuna? tuna tatizo, nchi inakwenda kwenye uchumi wa kati kuna kundi kubwa la watu ni wavivu sana huo ndiyo ukweli - Spika Ndugai

• Inauma hata timu yetu ya Taifa ikienda kucheza huko wachezaji hawajitumi, Watanzania hawafanyi kazi huoni hata wakilitafuta goli kama wenzao wanavyojituma, inabidi tubadilishe mitazamo ili vijana wetu hawa wachangamke na wapende kazi - - Spika Ndugai
#BinagoUPDATES

No comments