Advertisement

Responsive Advertisement

WANUNUZI WA KOROSHO WAPEWA ONYO KALI

Waziri wa Kilimo Prof Adolf Mkenda ametoa onyo kali kwa wanunuzi wa korosho kwa njia isiyo halali maarufu kama ‘Kangomba’ hali inaweza kusababisha wakulima kushindwa kuendelea kulima zao hilo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya maafisa ushirika yanayojumuisha mikoa mitano yanayofanyika mkoani mtwara amesema kuwa lazima wakemee ili kumsaidia mkulima.

Amesema kuwa serikali ina mikakati ya kuwezesha wakulima ili waendelee kulima zao hilo ambapo wanatoa pembejeo na kuwawezesha kwa namna mbalimbali ikiwemo kuimarisha ushirika na kuwawezesha maafisha ushirika na ugani ili kuwezesha zao hilo kuendelea kufanya vizuri.

Post a Comment

0 Comments