Jeshi la polisi mkoani Pwani linamshikilia, Anthony Lugendo mkazi wa Mlandizi mkoani humo kwa tuhuma za kumdhalilisha mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu.
Akizungumza na Binago Blog jana Ijumaa Septemba 17, 2021 mjini Kibaha Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa amesema tukio hilo limetokea Jumatano katika kitongoji cha Kaloleni kata ya Janga mkoani humo.
"Tulipata taarifa hiyo kutoka kwa raia wema tukafanya haraka kwenda eneo la tukio na tukamkuta mkazi huyo akiendelea na unyanyasaji huo tukamamata, " amesema.
Amebainisha kuwa walimkuta mtuhumiwa huyo akiwa chumbani kwake amemvua nguo zote mtoto huyo anayesoma shule ya awali.
Ameeleza kuwa hivi sasa wanamshikilia mkazi huyo wakiendelea na hatua mbalimbali kabla ya kumfikisha mahakamani.
Katika hatua nyingine Wankyo amesema wamekusanya Sh119,130,000 za faini 3, 971 za makosa ya usalama barabarani.
& MR. PM.✍
0 Comments