Akiwa nchini humo, Mhe. Rais Samia atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Rais Evariste Ndayishimiye, kisha atashuhudia utiaji saini wa hati za makubaliano na kuzungumza na vyombo vya habari.
Aidha, Mhe. Rais Samia atahudhuria na kuhutubia mkutano wa jukwaa la Wafanyabishara wa Burundi na Tanzania kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayohusu fursa za biashara na uwekezaji zilizopo nchini Tanzania na Burundi.
0 Comments