AMKA NA BWANA LEO 4

KESHA LA ASUBUHI

IJUMAA, JUNI, 4, 2021
SOMO: MTU AWAYE YOTE ASIWADANGANYE 

Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.

2 Timotheo 4: 3, 4. 



Kabla na wakati wa kuja kwa Kristo mara ya kwanza, walimu wa kidini walifundisha mafundisho mageni yaliyokuwa yamechanganywa na sehemu za ukweli ambayo yalikuwa na uwezo mkubwa wa udanganyifu, na yakazipotosha roho kutoka kwa Mungu, ingawa bado walikuwa wana mwonekano kuwa ni waabudu wa kweli wa Mungu. Tunaiona hali hiyo hiyo kwenye jamii katika siku hizi za mwisho, na wale wanaojitenga na imani, wanachanganya imani yao na maoni mbalimbali ya wanadamu. 



Biblia inakosolewa. Je, ni kwa sababu Maandiko hayapo thabiti na yanajichanganya kiasi kwamba wachungaji wanatofautiana sana katika kuitafsiri? Hapana, tatizo ni kwamba wanadamu wanafanya leo kama walivyofanya wakati wa Kristo, na wanafundisha mafundisho ya wanadamu. Walimu wa dini wapo katika hali ile ile kama ya Mafarisayo ambao aliwaambia, “Mwapotea, kwa kuwa hamyajui Maandiko wala uweza wa Mungu.” (Mathayo 22:29), Watu hawa ambao waliambiwa maneno haya walidhaniwa kuwa wanafundisha na kutafsiria watu Maandiko. 



Je, Maandiko hayako wazi na sio thabiti? Je, kuna msingi wowote unaoleta maoni yanayopingana na kauli mbalimbali na mafundisho ambayo yanasadikiwa katika ulimwengu wa dini? Ikiwa ndivyo hivyo, basi tunaweza kukaribisha mashaka juu ya asilia yake ya kiungu, maana si Roho wa Mungu anayewaongoza watu kuwa na maoni yanayotofautiana. 



Wale ambao wanafanya kazi ya kutafsiri Biblia, wamelipotosha Neno la Mungu na wameyapotosha Maandiko mbali na maana yake ya kweli, kwa kutafuta kuweka muafaka kwenye ukweli wa Mungu na mavumbuzi na mafundisho ya wanadamu. Maandiko yamepotoshwa na kutumiwa vibaya, thamani ya ukweli umewekwa katika mfumo wa makosa. Walimu hawa wamepofushwa, na hawawezi kuelewa kwa udhahiri maana ya kweli ya Maandiko.... 



Yesu, ambaye alitoa maisha Yake ili kuwaokoa wanadamu, ametupatia onyo kuhusu yale yatakayotokea katika siku za mwisho. Wanafunzi walimfuata wakiwa peke yao kumuuliza kuhusu mwisho wa dunia, na Yesu akasema: “Angalieni, mtu asiwadanganye. Sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.” (Mathayo 24:4, 5).



—Signs of the Times, Juni 4, 1894.


No comments