Advertisement

Responsive Advertisement

TAMKO LA DOROTHY KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA HEDHI

TAMKO LA WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO MHE. DKT. DOROTHY GWAJIMA (MB) KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA HEDHI SALAMA DUNIANI TAR. 28 MEI 2021

"Jamii bado inatakiwa kupiga hatua kubwa ya kuendelea kutoa elimu shuleni, katika jamii na pia nyumbani ikiwemo kuwashirikisha akina Baba
kutambua umuhimu wa hedhi salama kwa ujumla wake."

"Baadhi ya jamii wana imani potofu kiasi cha
kuwa na unyanyapaa na hivyo kuwa ni ngumu kuweka mipango ya maendeleo ya kuboresha usafi na hedhi salama hapa Nchini. Ni wakati muafaka sasa jamii kuachana na imani hizo na kukubali kuwa suala la hedhi ni sehemu ya maisha ya kawaida kabisa ya msichana au
mwanamke na ni jambo la baraka za Kimungu katika kuweka mfumo wa kuendeleza vizazi."

"Msichana au Mwanamke anapokuwa katika siku zake anatakiwa kuwa katika mazingira salama na kwamba anapata huduma zote muhimu ikiwemo miundombinu ya vyoo vyenye usiri, maji safi,
taulo za kike au vifaa salama vya kujisitiri na utupaji salama wa vifaa/taulo za kikebzilizotumika."

"Hedhi isiyo salama ina athari mbalimbali za kiafya ambazo ni pamoja na kupata magonjwa kama maambukizi katika mfumo wa mkojo yanayoweza kusambaa zaidi na kupelekea maam-
bukizi kwenye mji wa uzazi na hadi kufikia ugumba. Vilevile, ukiacha athari za kiafya, hedhi isiyo salama inaweza kuathiri maendeleo ya mwanamke katika nyanja zote ikiwemo elimu, uchumi, n.k."

"Nimechukua hatua ya kuvunja ukimya nawe chukua hatua hii ili kwa pamoja tuungane kuelimisha na kuhamasisha jamii kuachana na mila na desturi potofu kuhusu hedhi na kuhaki-
kisha wanaungana kuratibu upatikanaji wa huduma na vifaa vya kujihifadhi hasa taulo za kike sehemu zote kwa makundi yote na hata
kuwa na bei elekezi katika bidhaa hii."





Post a Comment

0 Comments