Advertisement

Responsive Advertisement

PART 3 NA MALISA GJ

Mmoja wa vijana hao Simon Mwacha alivunjwa mkono karibu na joint. Hadi sasa amefanyiwa upasuaji mara 3 lakini hajapona. Wiki iliyopita viongozi wa BAVICHA walimtembelea na kumkuta amewekewa POP jingine. Huu ni mwezi wa 7 tangu avunjwe na Sabaya na bado hajapona.

Kutumia number za UN kufanya uhalifu ni doa katika diplomasia ya nchi, lakini hakujali hilo. Yeye ni mtoto pendwa wa mwendazake, mtamfanya nini? Kama PM alishindwa kumfanya lolote, aliamini wengine hawamuwezi.

Aliwekeza nguvu na akili zake zote kwa mwendazake. Alimtumainia, alimuabudu na kumsujudu. Lema aliwahi kumwambia huyo unayemtegemea si Mungu. Ipo siku hatakuwepo na utakosa mtetezi. Sabaya akacheka kwa dharau. Leo yametimia yale aliyosema Lema miaka mitatu iliyopita.

Sabaya anatuhumiwa kumteka na kumpiga mtia nia wa udiwani huko Machame. Anatuhumiwa kunyanyasa wananchi mbalimbali kwa sababu za kisiasa. Anatuhumiwa kumpiga ngumi na kumpasua uso mfanyabiashara (Shoo) wa Bomang'ombe baada ya kumkuta akiuza vileo kwenye duka la bidhaa za rejareja.

Sabaya alitengeneza kikundi cha "mabaunsa" ambacho kilikua kinatembea nae popote. Hawakua walinzi rasmi wa serikali. Ni "wahuni" tu aliowaokota mtaani na kuwapa silaha, kama alivyofanya(ga) Bashite.

Kikundi hiki kilikua hakina tofauti na "Mungiki" maana kilitii kila order ya boss wao, hata ambazo ni unlawful. Kiliteka, kilijeruhi na kiliharibu mali kwa order ya Sabaya. Kikundi hiki kiliwahi kuteka moja ya magari ya Freeman Mbowe (likiwa imepaki Arusha) na kutia chumvi kwenye engine. Pamoja na Mbowe kuripoti polisi lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa.

Kitendo cha Sabaya kuokota vijana mtaani wasio na mafunzo yoyote ya kijeshi na kuwapa silaha wamlinde ni kosa kisheria. Lakini nani wa kuhoji kama mwendazake alibariki hilo?

Kikundi hiki kimewahi kumpiga mfanyabiashara mmoja (Molel) pub moja maeneo ya Kijenge. Vijana wa Sabaya walimzingira na kumtuhumu kumshika "makalio" mpenzi wa mmoja wao. Wakampiga na kumlazimishwa kutoa kiasi cha pesa ili wamwachie. Kitendo hicho kiliharibu biashara ya eneo hilo, hadi sasa pamepoa licha ya kwamba ni eneo zuri la starehe.

Post a Comment

0 Comments