*KESHA LA ASUBUHI.*
Jumanne, 25/05/2021.
*KAA KATIKA KIVULI CHAKE.*
*Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe. Waefeso 4:11, 12.*
▶️Mungu hajamfanya mtu yeyote kubeba mzigo wa kazi peke yake. Amewaweka pamoja watu wenye uwezo tofauti, ili waweze kushauriana na kusaidiana. Kwa njia hii upungufu wa uzoefu na uwezo wa mtu mmoja unajaziwa kwa uzoefu na uwezo wa mwingine. Sote tunapaswa kujifunza kwa makini maelekezo yaliyotolewa katika Wakorintho na Waefeso kuhusu uhusiano wetu sisi kwa sisi kama washirika wa mwili wa Kristo.
▶️Katika kazi yako, Edson, unapaswa kuzingatia uhusiano ambao kila mfanyakazi anaudumisha kwa wafanyakazi wengine kuhusiana na utume wa Mungu. Unapaswa kukumbuka kwamba watu wengine na wewe mwenyewe pia mna kazi ya kufanya kuhusiana na mpango huu. Hupaswi kuzuia mashauri kuingia katika akili yako....
▶️Tumeunganishwa na huduma na utume wa Mungu, na kwa nafasi binafsi tunapaswa kutambua kwamba sisi ni sehemu ya kitu kizima kikubwa. Tunapaswa kutafuta hekima kutoka kwa Mungu, tujifunze kile kinachomaanisha kuwa na roho ya kusubiri, kukesha na kwenda kwa Mwokozi wetu tunapokuwa tumechoka na kufadhaika. Mwamini Mungu, na si katika hekima ya mwanadamu pekee.
▶️Unapaswa kujifunza kusalimisha nia na njia yako, na upokee nuru kutoka kwa wale ambao Mungu amewafanya kuwa mkono Wake wa usaidizi, wale ambao amefanya ili uweze kusaidiwa. Nenda kwa Kristo kwa ajili ya kupata pumziko. Mng’anganie. Kaa kwa muda mrefu kadiri iwezekanavyo ili usalimishe nia yako kwa mapenzi ya Mungu. Watu wengi wanakuwa na haraka sana kwenye maombi. Kwa hatua za haraka wanapita katika kivuli cha uwepo wa Kristo, wakipumzika pengine kwa muda mfupi ndani ya mazingira matakatifu, lakini hawasubiri mashauri.. Hawana muda wa kukaa chini, hawana muda wa kubaki na Mwalimu Mkuu. Wakiwa bado na mizigo yao, wanarudi kazini kwao....
▶️ *Kaza macho yako kwa Mwokozi. Jitenge na masumbufu ya dunia, na kaa chini ya kivuli cha Kristo. Unapaswa kufanya hivi na utapokea baraka tele, anasubiri kukupatia. Weka mawazo yako kwenye mambo ya juu na matakatifu. Kisha, katikati ya masumbufu na mgogoro wa kila siku, nguvu zako za kiroho zitahuishwa.*
*MUNGU ATUBARIKI SOTE.*
🙏🙏🙏🙏
0 Comments