KESHA LA ASUBUHI
JUMAPILI, MEI, 16, 2021
SOMO: KUJITOA KIKAMILIFU
Nimesulibiwa pamoja na Kristo, lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.
Wagalatia 2:20.
Mungu hatakubali kitu chochote pungufu ya kujitoa kikamilifu. Wakristo wanaojitoa nusu nusu, wenye dhambi kamwe hawaendi mbinguni. Huko hawatapata furaha; maana hawajui chochote kuhusu kanuni ya juu, takatifu ambayo inawaongoza wanafamilia wa familia ya kifalme.
Mkristo wa kweli daima anaacha wazi madirisha ya roho yakiwa yamefunguliwa kuelekea mbinguni. Anaishi kwa kufanya ushirika na Kristo. Nia yake inapatana na mapenzi ya Kristo. Shauku yake kubwa kabisa ni kufanana na Kristo zaidi na zaidi.....
Kwa bidii bila kuchoka tunapaswa kujitahidi tufikie kiwango ambacho Mungu anataka tuwe. Hatufanyi hivi kama malipo, bali kama njia pekee ya kupata furaha ya kweli. Njia pekee ya kupata amani na furaha ni kuwa na uhusiano hai pamoja Naye Aliyeyatoa maisha yake kwa ajili yetu, ambaye alikufa ili tuweze kuishi, na ambaye anaishi ili kuunganisha uwezo Wake pamoja na jitihada za wale ambao wanajitahidi kushinda.
Utakatifu ni kudumu kupatana na mapenzi ya Mungu. Je, hatupaswi kujitahidi tuwe vile ambavyo Kristo anatamani sana tuwe —wakristo katika matendo na ukweli —ili ulimwengu uweze kuona kwenye maisha yetu ufunuo wa uwezo uokoao wa ukweli? Dunia hii ni shule yetu ya maandalizi. Tunapokuwa hapa tutakutana na majaribu na magumu. Daima adui wa Mungu atatafuta kututenganisha na Kristo. Lakini tunapong’ang’ania kwa yule ambaye alijitoa kwa ajili yetu, basi tupo salama.
Ulimwengu wote ulikuwa umekusanyika ili kumkumbatia Kristo. Alikufa msalabani ili kumharibu yeye ambaye alikuwa na nguvu ya mauti, na kuiondoa dhambi ya kila roho iaminiyo. Anatuita tujitoe kwenye madhabahu ya huduma, kafara hai inayoteketeza. Tunapaswa kujitoa kikamilifu kwa Mungu pamoja na vitu tulivyo navyo na vile tulivyo.
Katika shule hii ya chini ya dunia tunapaswa kujifunza masomo ambayo yatatuandaa kuingia katika shule ya juu, mahali ambapo elimu yetu itaendelea chini ya mafunzo ya Yesu mwenyewe. Kisha atatufunulia maana ya Neno Lake. Je, katika siku chache hizi za mlango wa rehema zilizosalia, kwa nini tusitende kama wanaume na wanawake ambao wanatafuta uzima katika ufalme wa Mungu, hata furaha ya milele?
—The Review and Herald, Mei 16, 1907.
0 Comments