AMKA NA BWANA LEO 06/10/2021

*KESHA LA ASUBUHI*

*_LEO NA MUNGU - Jumatano, Oktoba 06, 2021_*

*_FANYA  MAZOEZI YA MBIO ZA KWENDA MBINGUNI_*

*_Na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe._ 1 Timotheo 5:4*

✍🏼 Imekuwa kawaida katika familia nyingi, kwa wazazi na vile vile kwa watoto, kuwapendeza zaidi wale wa jamii nyingine kuliko wale wa nyumbani kwao. Huu sio mpango ambao Mungu ameupanga kwa wazazi na kwa watoto. 

Tunza baadhi ya tabasamu zako na sifa na adabu kwa ajili ya mazingira ya nyumbani kwako. Inakupasa kujitahidi kuwa mpole, mwenye kufikiria, mwenye fadhili, kuonyesha adabu ya Kikristo nyumbani. 

*Roho ya neema ya dini ya nyumbani inapaswa kupaliliwa.*

✍🏼 Kristo hakuwahi kuzungumza neno kali au lisilo na fadhili. Hata alipojaribiwa na washirika wake kutenda mabaya, aliimba Zaburi, au kwa kutumia baadhi ya maneno ya maandiko alimkatisha tamaa adui. Msione haya kujifunza kwa Kristo. Anawaalika, *_"Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi” (Mathayo 11:29, 30)._*

 Wakati unapohisi kusukumwa kukasirika zingatia hili katika kudhihirisha roho hii, hauivai nira ya Kristo, ambayo ni moja ya utii, kujizuia, huduma.

✍🏼 Wazazi na watoto, zingatieni hili, kwamba wafuasi wa kweli wa Kristo watazifanya nyumba zao kuwa kama mfano wa nyumba ya juu, kwa kufanya hivi wanakuwa watenda kazi pamoja na Kristo kutekeleza sheria za ufalme wake.

 Liishi ombi hilo. Hili ndilo hubiri lote kwa wale watakaolitendea kazi. 

👉🏽Tunalo jambo la kumwuliza Yesu. 
👉🏽Tuna mahitaji makubwa na matakwa makubwa, ambayo Kristo pekee anaweza kutupatia. 
👉🏽Ombi ambalo Kristo aliwafundisha wanafunzi wake linashughulikia haya yote. 
👉🏽Tunahitaji rehema, msamaha; lakini tunaweza kuyapata haya kama tukiwarehemu na kuwasamehe wengine.

🔘 *Kristo anaukaribisha ujasiri wako. Kwa wewe peke yako huwezi kufanya chochote. Huwezi kuwa mwema, mkweli, mwenye adabu, asiye na ubinafsi, bila msaada wa Roho Mtakatifu.... Jifunze maisha ya Kristo, na yafanyie kazi katika maisha ya nyumbani yale mambo ambayo unajua yatahitajika kwako katika maisha ya mbinguni, katika jamii ya familia ya mbinguni. Katika mazingira ya nyumbani hapa tunaweza kutengeneza tabia zetu kwa ajili ya familia ya juu.*

*MUNGU AKUBARIKI SANA*

No comments