Polisi katika Kaunti ya Baringo wanamshikilia mkuu wa shule ya upili anayedaiwa kumtupa moto mtoto wake wa miezi mitano na kumsababishia majeraha mabaya.
Paul Kipsang, ambaye ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Katokon huko Tiaty, anaripotiwa kumtia moto mtoto huyo nyumbani kwake katika eneo la Ngaratuko chini ya hali isiyojulikana.
Kulingana na Kamanda wa Polisi wa Kaunti Ndogo ya Baringo Kaskazini Fredrick Odinga, mshukiwa alikuwa amejificha na alikamatwa Jumatatu usiku, siku tano tangu baada ya kufanya kitendo hicho kibaya.
Mtoto amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Baringo ambapo anauguza uchomaji wa uso na sehemu za mwili.
Mama wa mtoto huyo aliwaambia polisi kuwa hapo awali mume alikuwa ametoa vitisho vya kuua kwa familia haswa anaporudi nyumbani akiwa amelewa.
Mshukiwa huyo alizuiliwa katika kituo cha polisi cha Loruk akisubiri kushtakiwa.
0 Comments