ITAFIKA SIKU AMBAPO HUTAJALI TENA-MWIJAKU

Inaweza kuwa Unaumia sana muda huu. Lakini itafika siku ambapo hutajali tena.

Itafika siku moja utapitisha siku nzima bila ya kumpigia simu au ku-mtext na kujiona uko sawa kabisa.

Itafika siku utasikia yupo na mtu mwingine na wala hutahisi kuumia au kukasirika.

Itafika siku moja, utaziona picha zake na wala hutajihisi jambo lolote. Unaweza kutana nae ukaongea nae na zile hisia za kuumiza juu yake hutazihisi tena.

Najua, unaweza usiamini ninachokiongea kutokana na tabia ya moyo ya kung'ang'ania, lakini, fahamu kwamba, muda nao huponya. Haiwezi kuwa hivi sasa, ila siku itafika tu.

Na siku hiyo itakapofika, utajishangaa kwanini ulikuwa ukilia? Kisha, utaona uamuzi wa kumuacha aende ulikuwa ni uamuzi wa busara katika maisha yako.

Usihofu, utafika hatua hiyo.

Holding on is believing that there’s only a past; letting go is knowing that there’s a future !

I care.

No comments