amka na bwana leo 15

KESHA LA ASUBUHI

JUMATATU, MACHI, 15, 2021
SOMO: MKRISTO MWENYE ADABU

Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

Waefeso 4:32. 



Tunahitaji kuhifadhi upendo katika mioyo yetu. Tusiwe tayari kuwafikiria uovu ndugu zetu. Ni lazima tuweke tafsiri kidogo sana juu ya kile wanachofanya au wanachosema. Ni sharti tuwe Wakristo wa Biblia. “Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo” (1 Petro 1:22). 



Hatupaswi kuwa wazembe kwa habari ya wokovu wa nafsi zetu wenyewe. “Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe” (2 Wakorintho 13:5). 



Hatupaswi kupita pasipo kujali. Ni lazima tuulize katika tabia ya mawazo na hisia zetu, tabia zetu, makusudi, maneno, na matendo. Hatuko salama ikiwa hatutadumu na kwa mafanikio kupigana vita dhidi ya upotovu wetu wenyewe wa dhambi. Ni lazima tuzingatie ikiwa sisi ni mfano wa utakatifu wa Kikristo, ikiwa tuko katika imani. Ikiwa hatutatafuta kwa bidii kuichunguza mioyo yetu katika nuru ya Neno la Mungu, kujipenda wenyewe kutatuchochea kufikia wazo zuri sana kuhusu sisi wenyewe kuliko ambavyo tungepaswa. 



Hatupaswi kuwa na bidii katika jitihada zetu wenyewe kuwaweka sawa wengine kiasi cha kutotilia maanani nafsi zetu wenyewe. Hatupaswi kuwa na bidii sana kwa ajili ya ndugu zetu na katika bidii hii tukaacha kujali kazi inayohitaji kufanywa kwa ajili yetu wenyewe. Kosa la mwingine haliwezi kufanya upande wetu kuwa karibu na sahihi. Kuna kazi binafsi inayopaswa kufanywa kwa ajili yetu binafsi, ambayo hatupaswi kuipuuza kabisa. 



Ikiwa tumejazwa na rehema na upendo wa Mungu, matokeo yanayolingana nayo itazalishwa kwa wengine. Hatuna chochote cha kujivunia. Vyote ni kipawa cha mpaji Mwokozi. Ni sharti tuhudumie nafsi zetu wenyewe kwa bidii. Ni lazima tutembee katika unyenyekevu. Hatutaki kuvaa mavazi ya vita, bali mavazi ya amani na haki. Hebu Bwana na atufundishe kuivaa nira yake na jinsi ya kuubeba mizigo yake. Kila jambo katika kusudi hili na kazi hii linaweza kukamilishwa kwa roho njema, inayopatanisha. Tunaweza kuwa wenye heshima, mara zote, na kamwe tusiogope kuwa hivyo zaidi sana. Ni lazima tujizoeze katika kutenda mema kwa watu 

No comments