Advertisement

Responsive Advertisement

FREEMON MBOWE KUELEKEA MWANZA KUDAI KATIBA MPYA

Kutokana na Jeshi la Polisi kuzuia Kongamano la Katiba lililokuwa limeandaliwa na Baraza la Vijana la Chademansiku ya Jana tarehe 17 Julai,2021 na kuwakamata Wanaharakati,Viongozi wa Dini, Viongozi wa Chama, wanachama,wananchi na watanzania Kwa ujumla ambao wanataka kupatikana Kwa Katiba Mpya nchini katika Jiji
la Mwanza.

Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe.Freeman Mbowe amelazimika kukatisha siku za Maombolezo ya Msiba wa Kaka yake Kijijini kwao Machame Moshi na ataelekea Jijini Mwanza Kwa ajili ya kushirikiana na Watanzania wote katika
kuhakikisha kuwa Haki ya kukusanyika na kujadiliana inapatikana Kwa mujibu wa Katiba ya Nchi.

Mwenyekiti wa Taifa Mhe.Freeman Mbowe atazungumza na Taifa akiwa Jijini Mwanza kesho tarehe 19 Julai,2021 saa tano kamili asubuhi .

Kwa hatua ya sasa Chama kinalaani vikali hatua ya Jeshi la Polisi ya kuwakamata na kuendelea kuwashikilia Watanzania hawa ambao kimsingi hakuna kosa lolote ambalo wamefanya Kwa mujibu wa Sheria zetu .

Tamko rasmi la mwelekeo na hatua ambazo Chama kitachukua zitatangazwa na Mwenyekiti wa Chama Mhe.Freeman Mbowe kesho jumatatu Jijini Mwanza .

Post a Comment

0 Comments