AMKA NA BWANA LEO 10
KESHA LA ASUBUHI
Jumatatu 10/05/2021
*KUWA HAI KATIKA MUNGU*
*Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.* Mathayo 10:32, 33
Hii inakuwaje? *Je, tunamkiri Kristo katika maisha yetu ya kila siku? Je, tunamkiri Yeye katika mavazi yetu, tunajivisha katika mwonekano wa kawaida na wa heshima? Je, mwonekano wetu ni ule wa roho ya upole na utulivu ambao ni wa gharama kubwa machoni pa Mungu? *Je, tunajitahidi kuiendeleza kazi ya Bwana wetu? Je, mpaka kati yako na dunia upo dhahiri, au unatafuta kufuata mitindo ya kizazi hiki kilichoharibika? Je, hakuna tofauti kati yako na dunia? Je, roho inayofanya kazi kwako ndiyo ile sawa na ya watoto wasiotii?*
*Ikiwa sisi ni Wakristo, tunamfuata Kristo, ingawa njia ambayo tunapaswa kuipitia inakata kwenye tabia zetu za asili. *Hakuna maana kukwambia kwamba hupaswi kuvaa hiki au kile, maana ikiwa upendo wa vitu hivi visivyo na maana upo ndani yako, kuacha kujipamba kutakuwa kama kukata tawi la mti*. Matamanio ya moyo wa asili yataibuka tena yenyewe. Unapaswa kuwa na dhamiri yako mwenyewe.
*Je, tunakumbuka kwamba Yesu alikuwa maskini, ili kwamba kupitia umasikini wake tuweze kuwa matajiri,* si jambo jema zaidi kutafuta kulitukuza jina lake na kuendeleza utume Wake? *Tunapaswa kukaa kwake kama tawi linavyokaa katika shina. Yesu anasema, *Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote... Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu" (Yohana 15:5—8).*
*Kama tungetimiza amri hii ya Bwana wetu, kungekuwa na hali tofauti ya mambo kwenye makanisa yetu, na tunapaswa kujua maana ya kujazwa na Roho wa Mungu. Kile tunachohitaji ni kuwa na shoka tayari kwenye mzizi wa mti. Tunapaswa tuifie dunia, tuifie nafsi, na kuwa hai kwa Mungu. Maisha yetu yanapaswa kuwa yake pamoja na Kristo katika Mungu, kwamba atakapoonekana sisi pia tutaonekana pamoja naye katika utukufu. Tunapaswa kuwa karibu na Kristo, ili watu waweze kujua kwamba tumekuwa na Kristo na kujifunza kuhusu Yeye... Kaza macho yako kwa Kristo. Kwa unyenyekevu wa roho tafuta kuwa karibu na Mungu. Katika maneno, katika matendo, mkiri Kristo.*
*MUNGU AKUBARIKI SANA MPENDWA*
Post a Comment